DHIMA YA MSIMULIZI KATIKA RIWAYA YA DUNIA UWANJA WA FUJO

503 Article Views All time
4600 Downloads All time
0 Citations Source: OpenAlex

Activity (views + downloads) over time

Citations by year

No citation data available yet.

Abstract

 Hadithi yoyote husimuliwa. Usimulizi huo hufanywa na msimulizi ambaye kwa hakika huwa tunaisikia sauti yake. Hata hivyo, katika kazi za fasihi andishi kama vile riwaya, sauti ya msimulizi huwa haisikiki kwa masikio kama ilivyo katika usimulizi wa simulizi za kimapokeo, bali wasomaji huweza kuisikia kwa kutumia akili zao wanapoisoma kazi husika (Mohochi, 2000). Sauti hii ya msimulizi inayosikika katika akili za wasomaji huwawezesha kubaini anayeongea na dhima anayoitekeleza katika kazi husika. Hivyo, makala haya yamejikita katika kubainisha dhima za msimulizi katika riwaya ya ' Dunia Uwanja wa Fujo ' ya Euphrase Kezilahabi.