
Wahusika wa Kitashtiti katika Gamba la Nyoka
Kiswahili
##common.published##: February 15, 2016
395
Article Views
All time
398
Downloads
All time
0
Citations
Source: OpenAlex
Activity (views + downloads) over time
Citations by year
No citation data available yet.
Abstract
Makala haya yanachunguza uumbaji wa wahusika katika Gamba la Nyoka ambayo ni mojawapo ya riwaya za Euphrase Kezilahabi. Tumewatambulisha wahusika wakuu watano ambao ni Mambosasa, Mamboleo, Padri Madevu, Mama Tinda na Mzee Chilongo. Hawa ndio wahusika ambao tunawachunguza. Lengo letu ni kudhihirisha kwamba uumbaji wa wahusika hawa umetumia mtindo wa kitashtiti. Mbinu za utunzi zinazohusishwa na tashtiti ni kama vile kinaya, ucheshi, dhihaka na bezo. Kwa vile tashtiti hudhamiriwa kukashifu na pia kupiga vita maovu ya kijamii, makala haya yanaangazia matumizi ya mbinu hizi katika kufanikisha lengo hilo.