Matumizi ya Alama za Kifonetiki za Kimataifa katika Uwasilishaji wa Taarifa za Kimatamshi katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu Toleo la 3
Abstract
Kamusi ni kitabu muhimu cha lugha ambacho hutoa taarifa mbalimbali kuhusiana na lugha fulani mahususi. Pamoja na kutoa maana ya neno, kamusi inatakiwa pia kutoa taarifa nyingine muhimu za kisarufi zikiwamo za kimatamshi (Wells, 1985). Uwasilishaji wa taarifa hizi za kimatamshi hutumia alama fulani za kifonetiki zinazowakilisha matamshi hayo. Kwa kutumia Nadharia ya Fonolojia Zalishi, makala hii inachambua Alama za Kifonetiki za Kimataifa (kuanzia sasa AKIKI) zilivyotumika kuwasilisha taarifa za kimatamshi katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu (2014) toleo la 3 (kuanzia sasa KKS3). Katika uchunguzi huu tunaeleza jinsi AKIKI zilivyotumika. Pia, makala hii inabainisha ubora na udhaifu wa matumizi ya AKIKI katika KKS3. Aidha, mapendekezo ya namna ya kunukuu matamshi kwa kutumia AKIKI yametolewa. Data za makala hii zimekusanywa kwa mbinu ya kusoma kamusi husika kwa umakini. Mbinu hii imetumika kwa kusoma KKS3 ambapo imechunguzwa jinsi taarifa za kimatamshi zilivyowasilishwa ili kubaini AKIKI zilivyotumika.
Downloads
Published
Issue
Section
License
Authors who publish in Kioo cha Lugha retain the copyright to their work and grant the University of Dar es Salaam a non-exclusive license to publish, reproduce, and distribute the article.
This article is published under the Creative Commons Attribution 4.0 International (CC BY 4.0) License, which permits unrestricted use, distribution, adaptation, and reproduction in any medium, provided the original work is properly cited.
