Athari za Mabadiliko ya Maana katika Lugha ya Kiswahili: Mifano kutoka Matini za Kidini
Abstract
Makala hii inachanganua matumizi ya lugha katika mahubiri ya kidini. Azma kuu ni kuchunguza jinsi maana za maneno zinavyobadilika kiisimu zinapotumiwa kwenye miktadha ya mahubiri ya Kikristo. Data ya utafiti imetokana na unukuzi kimaandishi wa vipindi 5 vya mahubiri ya Kikristo yaliyorekodiwa kati ya Mei na Agosti, 2020 kutoka idhaa tatu za runinga nchini Kenya, yaani KBC, SAYARE na MBCI. Wahubiri 5 waliotumia Kiswahili tu kwenye vipindi vya idhaa hizi ndio walioteuliwa kwa usampulishaji kusudio. Data ya semi 64 zilizoteuliwa kwa usampulishaji huo zilichanganuliwa kwa mwongozo wa madhumuni ya utafiti pamoja na mihimili ya Nadharia ya Pragmatiki Leksika. Matokeo yanaonesha kwamba baadhi ya maneno yaliyotumiwa na wahubiri wa dini za Kikristo huwasilisha maana kipragmatiki. Maana za maneno hayo kimatumizi ni tofauti na maana msingi. Aidha, uchunguzi huu unaazimia kuendeleza mtazamo wa isimu kuhusu jinsi matumizi ya lugha katika muktadha wa sajili hii maalumu unavyoathiri mawasiliano.
Downloads
Published
Issue
Section
License
Authors who publish in Kioo cha Lugha retain the copyright to their work and grant the University of Dar es Salaam a non-exclusive license to publish, reproduce, and distribute the article.
This article is published under the Creative Commons Attribution 4.0 International (CC BY 4.0) License, which permits unrestricted use, distribution, adaptation, and reproduction in any medium, provided the original work is properly cited.
