Mabadiliko ya Utambulisho wa Mwanamke na Uimarishaji wa Ujinsuke
Mifano kutoka Riwaya ya Nyuso za Mwanamke (Mohamed, 2010)
Abstract
Tafiti mbalimbali kuhusu riwaya ya Kiswahili zinaonesha kuwa mwanamke amesawiriwa kwa mitazamo mbalimbali, ukiwamo mtazamo hasi. Usawiri wa mtazamo huo unamtambulisha mwanamke kama kiumbe dhaifu na duni. Kwa kuongozwa na Nadharia ya Udenguzi, makala imeonesha namna mhusika mwanamke anavyoweza kubadilisha utambulisho hasi na kujenga utambulisho chanya. Makala imetumia data kutoka katika riwaya ya Nyuso za Mwanamke (Mohamed, 2010) zilizopatikana kwa usomaji makini. Makala imeweka bayana nafasi ya riwaya ya Kiswahili katika kujenga utambulisho wa mwanamke unaoimarisha ujinsuke. Matokeo haya yanatokana na uumbaji wa wahusika wanawake wanaodengua kaida za jamii zinazomkandamiza mwanamke na kufichua mbinu zinazotumiwa na baadhi ya wanajamii kuendeleza ukandamizaji huo. Pia, umuhimu wa wanawake kujitambua na kujisimamia umewekwa bayana.
DOI: https://dx.doi.org/10.4314/kcl.v22i2.3
Downloads
Published
Issue
Section
License
Authors who publish in Kioo cha Lugha retain the copyright to their work and grant the University of Dar es Salaam a non-exclusive license to publish, reproduce, and distribute the article.
This article is published under the Creative Commons Attribution 4.0 International (CC BY 4.0) License, which permits unrestricted use, distribution, adaptation, and reproduction in any medium, provided the original work is properly cited.
