Michakato ya Kisintaksia ya Uundaji wa Sentensi Changamani za Kiswahili
Abstract
Makala hii inalenga kuchambua michakato ya kisintaksia ya uundaji wa sentensi changamani za Kiswahili kwa kubainisha namna kishazi kikuu na kishazi bebwa vinavyowekwa pamoja kuunda sentensi hizo. Ili kufanikisha lengo hilo, makala imeongozwa na Nadharia Rasmi ya Chomsky (1965). Data za makala hii ni sentensi changamani za Kiswahili ambazo zilikusanywa kwa njia ya usomaji wa matini kutoka katika riwaya na magazeti. Matini hizi ziliteuliwa kwa kutumia mbinu ya usampulishaji nasibu sahili. Uchambuzi wa data ulifanyika kwa mkabala wa kitaamuli kwa kutumia mbinu ya uchambuzi wa kimaudhui. Makala hii imebaini kwamba kuna michakato mitatu inayotumika kuunda sentensi changamani ambayo ni uchopekaji, udondoshaji-chopezi na udondoshaji-chopezi hamishi. Kwa kutumia Nadharia Rasmi, imebainika kwamba kila mchakato una hatua zake katika kuunda sentensi changamani.
Downloads
Published
Issue
Section
License
Authors who publish in Kioo cha Lugha retain the copyright to their work and grant the University of Dar es Salaam a non-exclusive license to publish, reproduce, and distribute the article.
This article is published under the Creative Commons Attribution 4.0 International (CC BY 4.0) License, which permits unrestricted use, distribution, adaptation, and reproduction in any medium, provided the original work is properly cited.
