Muundo wa Mashairi katika Diwani ya Mnyampala (1965) na Nafasi yake katika Kuibua Maudhui
Abstract
Makala hii inachambua muundo wa mashairi katika Diwani ya Mnyampala (1965) na nafasi yake katika kuibua maudhui. Lengo ni kuangalia vipengele vya muundo vinavyojitokeza katika diwani hii. Vipengele vilivyoshughulikiwa ni mishororo, beti, mizani, vina, kituo au kibwagizo na mkarara. Pia, tunaangalia muundo huo ulivyotumika kuibua dhamira mbalimbali za kisiasa, kijamii na kiuchumi katika diwani hiyo. Makala hii pia inadadisi namna mbinu za kimuundo zilivyofanikisha usawiri na ubainishaji wa falsafa ya mtunzi kuhusu ushairi wa Kiswahili na nafasi ya ushairi katika jamii. Makala imeanza kwa kugusia usuli wa historia ya ushairi wa Kiswahili, historia fupi ya maisha ya Mathias Mnyampala na nadharia yake kuhusu ushairi wa Kiswahili. Data za makala hii zimepatikana kwa kusoma matini husika na kuchambua vipengele vyake vya kimuundo.
Downloads
Published
Issue
Section
License
Authors who publish in Kioo cha Lugha retain the copyright to their work and grant the University of Dar es Salaam a non-exclusive license to publish, reproduce, and distribute the article.
This article is published under the Creative Commons Attribution 4.0 International (CC BY 4.0) License, which permits unrestricted use, distribution, adaptation, and reproduction in any medium, provided the original work is properly cited.
