Ubabedume katika Ushairi wa Kiswahili: Mfano wa Utenzi wa Fumo Liyongo
Abstract
Suala la uana limepewa kipaumbele miongoni mwa masuala yanayotafitiwa katika taaluma mbalimbali zinazohusu maisha ya binadamu. Majukumu ya jinsi ya kike na jinsi ya kiume ni suala ambalo linaendelea kuzua mgogoro miongoni mwa watu wa jamii mbalimbali. Hata hivyo, utafiti wa uana unaozingatia jinsi ya kiume katika Kiswahili, hususan fasihi simulizi haujashughulikiwa kwa kina. Tafiti nyingi zilizopo zimeshughulikia masuala ya kike. Kuna haja ya utafiti kufanywa kuhusu suala la jinsi ya kiume katika fasihi, hususan katika ushairi wa jadi wa Kiswahili. Makala haya yanachunguza suala la ubabedume katika Utenzi wa Fumo Liyongo kwa kuzingatia majukumu, sifa na nafasi ya mwanamume katika utenzi huu. Makala yameongozwa wa nadharia ya ubabedume inayosisitiza maumbo ya vitambulishi vya jinsia ya kiume kwa kuzingatia jamii, maandishi na matukio au maelezo ya kihistoria.
Downloads
Published
Issue
Section
License
Authors who publish in Kioo cha Lugha retain the copyright to their work and grant the University of Dar es Salaam a non-exclusive license to publish, reproduce, and distribute the article.
This article is published under the Creative Commons Attribution 4.0 International (CC BY 4.0) License, which permits unrestricted use, distribution, adaptation, and reproduction in any medium, provided the original work is properly cited.
