Wahusika wa Kitashtiti katika Gamba la Nyoka

307 Article Views All time
1758 Downloads All time
0 Citations Source: OpenAlex

Activity (views + downloads) over time

Citations by year

No citation data available yet.

Abstract

Makala hii inachunguza uumbaji wa wahusika katika Gamba la Nyoka ambayo ni mojawapo ya riwaya za Euphrase Kezilahabi. Tumewatambulisha na kuwachunguza wahusika wakuu watano ambao ni Mambosasa, Mamboleo, Padri Madevu, Mama Tinda na Mzee Chilongo. Lengo letu ni kudhihirisha kwamba uumbaji wa wahusika hawa umetumia mtindo wa kitashtiti. Tashtiti ni mbinu pana inayojumuisha mbinu nyingine kadha (Wamitila, K.W. 2003:223). Hata hivyo, ili kuondoa uwezekano wa kukanganya, tunaweza kuzichukulia mbinu kama vile kinaya, ucheshi, dhihaka na bezo zinazotumiwa kuiunda kama vijenzi vyake. Kisawe cha istilahi tunayoizungumzia kwa lugha ya Kiingereza ni satire. Kwa vile tashtiti hudhamiriwa kukashifu na pia kupiga vita maovu ya kijamii, makala hii inaangazia matumizi ya mbinu hizi katika kufanikisha lengo hilo.